c Isa 30:28; 42:14; 64:12; 29:6; 65:6; Za 18:8; 107:25; 96:13; 83:15; 147:18; Ay 37:9; Yn 1:4; Nah 1:3
Psalms 50:1-6
Ibada Ya Kweli
(Zaburi Ya Asafu)
1 aMwenye Nguvu, Mungu, Bwana,
asema na kuiita dunia,
tangu mawio ya jua
hadi mahali pake liendapo kutua.
2 bKutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu,
Mungu anaangaza.
3 cMungu wetu anakuja na hatakaa kimya,
moto uteketezao unamtangulia,
akiwa amezungukwa na tufani kali.
4 dAnaziita mbingu zilizo juu,
na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
5 e“Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu,
waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
6 fNazo mbingu zinatangaza haki yake,
kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Copyright information for
SwhKC